Monday, 27 February 2017

NOKIA 3310 MPYA NI KAMA WINE YA ZAMANI KWENYE CHUPA MPYA ZIFAHAMU SIFA ZA NOKIA 3310 TOLEO LA SASA


Kwa Mara ya kwanza Nokia 3310 ilizinduliwa mwaka 2000 huku wakiuza simu milioni 126 duniani kote nahuifanya kuwa simu iliouzika zaidi duniani
Nokia wameamua kuturudisha kwenye miaka ya 2000 kipindi ambacho kwa hapa kwetu inchini Nokia 3310 ilikuwa ikiitwa jeneza kutokana na muundo wake ulivyo kuwa.

Simu hiyo imezinduliwa na HMD global , ambao ndio wenye haki ya mauzo ya brand ya Nokia. Lack ni je ni kwa kiasi gani Nokia 3310 ya 2000 inafanana na hii iliozinduliwa sasa , hiki ndio kila kitu unacho takiwa kukijua

TAREHE YA KUZINDULIWA
Imezinduliwa tarehe 26  February katika MOBILE WORLD CONGRESS 2017(MWC 2017)  mjini Barcelona , haijajulikana ni lini simu hii itaanza kuuzwa lakini taarifa ni kwamba itaanza kuuzwa robo ya muhula wa pili wa 2017

BEI
Inadaiwa simu hii mpya itapo ingia sokoni itakuwa na gharama ya £49 , mwanzoni ilidaiwa zitauzwa kwa £129

MUUNDO 

Nokia 3310 impya inabakia na muundo wake ule ule wa zamani wa kuwa na keyboard pamoja na kio ambacho hakina uwezo wa screen touch kama smartphone za sasa. Pia maza board ya simu hii mpya ni kama ule wa zamani tofauti ya sasa ni nyembamba na nyepesi kuliko toleo la 2000
Toleo la sasa pia linakuja na rangi ya nyekundu, njano na dark buluu.

DISPLAY
Toleo la nyuma display Yake ilikuwa haioneshi rangi lakini toleo la sasa display Yake ina ukubwa wa inchi 2.4 huku ikiwa na rangi , taarifa ya HMD ni kwamba display imetengenezwa kirahisi isiyokuwa na mwanga Mkali sana mahususi kwa ajili ya kutunza chaji ya betri la simu.

SIFA NYINGINEZO
Nokia 3310 toleo la sasa pia linakuja na betri lenye nguvu ya 1200mAh ambalo lanaweza Toka kwenye simu, linauwezo wa masaa 22  ya maongezi na mwezi mzima wa kuwa na chaji , ndio umesoma sawa simu hiyo inauwezo wa kukaa na chaji mwezi mmoja .
Pia toleo la sasa linakuja na camera yenye megapixel 2.0 , 16MB memori ya ndani ya simu pia kuna sehemu ya kuweka memori kadi yenye uwezo hadi 32 GB , Nokia 3310 toleo la sasa unaweza ukatimia Internet  yenye uwezo wa 2G.

Kwa wale wapenzi wa game la nyoka pia nalo lipo na likiwa limeongezewa manjonjo

Pia  Nokia wametangaza matoleo mengine ya Nokia ambayo yameanza kuuzwa kwenye soko la China ambayo ni Nokia 6 , 5 na 3 kaa karibu na blogu hii utapata sifa za simu zote hizo.

TECNO L9 NA L9 PLUS NI TOLEO LIJALO KWA SIMU ZA TECNO


Tetesi ni kwamba Tecno wanategemea kuleta wanafamilia wengine kwenye series ya L ambao si wengine ni L9 na L9 plus , kwa tetesi ni kwamba zinakaribia kuzinduliwa hivi karibuni.
Simu za tecno katika familia ya L Series zina aminika kwa utunzaji wake wa betri kwakuwa zinawekewa betri zenye nguvu kubwa kama tuliovyoona kwenye L8 na L8 plus zilozo kuwa na betri zenye nguvu ya 5050 mAh. Kwa hiyo tutegeme vivyo hivyo kwenye tecno L9 na L9 plus.

Sifa nyinginezo za kutegemea ni muundo bora kabisa pamoja na mabadiliko katika software , pia kwa upande wa  RAM L9 inategemewa kuwa na 2GB wakati L9 plus ni 3GB RAM.
Pia simu hizo zinatarajiwa kuja pamoja na Android version ya sasa ya 7.0 nougat.

Kuwa karibu na blogu hii kupata sifa zote za simu hizo pindi tu zitapo toka.

Thursday, 2 February 2017

FAHAMU SIFA ZA SMARTPHONE MPYA YA ITEL S31


Itel wamekuletea smartphone nyingine katika familia ya S series. Baada ya toleo la kwanza la itel s11 sasa waneleta mwanafamilia mwingine ambaye ni itel s31.
Katika series ya S , itel wamejikita katika kukupa smartphone yenye uwezo wa kukupa picha nzuri pale unapojipiga SELFIE yako.
Itel s31 ni smartphone yenye muundo mzuri na muionekano bora kabisa pia ushikakapo mkononi mwako ina texture nzuri kwenye mfumuko wa simu nyuma. Kona za s31 ni round katika pembe zote nne za simu
Itel s31 inaukubwa wa  inch 5.5 IPS HD DISPLAY na wembamba wa  8.7mm ambao unaipa smartphone hiyo muonekano wa wembamba  unapoishika mkononi na pia ni rahisi kupokonyoka mkononi lakini s31 inakuja pamoja na kava.

Sifa zinginezo za itel s31

IMETANGAZWA: January 2017
UPATIKANAJI: February 2017
RANGI: Black, Rose Gold and Champagne Gold.
SIM KADI: ni mbili (sim kadi ndogo na ya kawaida)
OS(OPERATING SYSTEM): ni Android 6.0 marshmallow
NETWORK: GSM, GPRS, EDGE, HSPA haina LTE(4G)
CPU: Quad-core 1.3 GHz processor
MEMORY: Memory ya ndani(ROM) ni 16GB  RAM ni 1GB
CAMERA: ina 5 megapixel ikiwa na uwezo wa autofocus pamoja na flash light, camera ya selfie pia ni 5 megapixel pia ikiwa na flash light kwa muonekano mzuri sehemu yenye mwanga hafifu
BETRI: lina ujazo 2400 mAh li-lon ambalo unaweza litoa.